The Voice --tunaifikia jamii kwa nyimbo za Injili



Kundi la Muziki wa Gospel la The Voice limesema kuwa litaendelea kutoa elimu zaidi ya Mungu kwa njia ya muziki.


Kundi hilo mwaka huu linatimiza miaka 20 tangia kuanzishwa kwake.


Kundi hilo linaloundwa na wanamuziki kutoka ukoo mmoja lilianza kufanya kazi zake za muziki tangia wakiwa watoto mwaka 1994 .


Akizungumza na safu hii Meneja wa kundi hilo, Obed Mark alisema kuwa wakiwa wanatimiza miaka 20 tangia kuanza kuimba wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kufikia idadi kubwa ya watu wa rika mbalimbali.


Alisema kuwa wanaimba muziki wa Injili wakitumia vionjo mbalimbali na wamekuwa wakipata mialiko kwenda katika hafla mbalimbali.


"Sisi kama unavyotuona tunaonekana kuwa ni bado wadogo kiumri sasa tukisema tunaadhimisha miaka 20 inamaanisha ni kuanzia pale tulipoanza kuimba tukiwa watoto na kwa sasa tunazidi kukua kwa kuongezeka pia hata kwenye kundi"alisema Mark.


Wanaounda kundi hilo ni pamoja na Obeid Mark, Mark Mark, Daniel Mark, Baraka Mark, Josia Bedock na Josia Magoth.

Related

Fahamu yaliyojiri majuzi kwenye tuzo za MTV, VMA Marekani

Na Evance Ng'ingoHIVI majuzi nchini Marekani ilifanyika hafla ya utoaji wa tuzo za  Video bora za wasanii za MTV. Tuzo hizo ambazo hutolewa kila mwaka zinalenga kuwatuza wasanii wa muziki...

Usajili waongeezwa tena mbele mwisho leo

Na Mwandishi WetuDIRISHA la usajili la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwa wachezaji wazalendo limesogezwa mbele kwa Saa 48 zaidi tangia juzi na hivyo leo ndi mwisho.Hatua hiyo ni kutokana na klab...

Watuhumiwa wa wizi wachomwa moto Tabata

Vijana wawili wamechomwa moto katika aneo la Tabata Lewiti wakituhumiwa kuiba pochi ya mwanamke katika eneo hilo. Walioshuhudia tukio hilo walisema kuwa lilitokea asubuhi ya jana (...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:

item