Bang Magazine yagonga miaka 10, yafanya sherehe, The Voice yaburudisha vema

Elgiver alifungua mvinyo
The Voice waliwakilisha
Mwanamuziki Yvone Sangudi ambae ni Mtanzania anaefanya shughuli zake za muziki Marekani alikuwapo
Mtoto anaimba huyu

Emelda Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Relim inayomiliki jarida la Bang (mwenye nyeusi) akijimwaga mwaga

Akiwa na friend

Pamoja na friends
Na Evance Ng'ingo
MSANII wa kitanzania aishie nchini Marekani Yvonne Sanguda pamoja na kundi la muziki wa Injili la The Voice juzi walifanya onesho zuri kwenye sherehe za kuadhimia miaka 10 ya jarida la Bang.


Katika sherehe hizo zilioandaliwa na kampuni ya Relim inayomilikia jarida hilo zilifanyika katika fukwe ya Escape One na kuhudhuriwa na maelfu ya watu.


Msanii Yvonne alianza kwa kuimba nyimbo zake kadhaa huku akiwa anacheza na kuimba kwa pamoja na  kuonesha uwezo wa hali ya juu katika kumudu jukwaa.


Aliendelea kucheza huku akiimba na kuna wakati alikuwa akikaa chini kwenye steji ambapo alikuwa akiimba muziki wa live akisaidiwa na bendi ya Tanzanite.


Baada ya hap likaja kundi la The Voice ambalo linaundwa na wasanii sita ambao waliomba wimbo maalum wa kulipongeza jarida hilo.


Walizikonga nyoyo za wageni waliohudhuria onesho hilo hasa kutokana na umahiri wao wa kuimba bila vifaa ila wakijitungia mapigo ya muziki wenyewe (Akapela).


Mwanadada Angel Magoti wa kundi hilo alikuwa ni mfano wa kuigwa kutokana na umakini wake katika kupanga sauti na kuimba kwa ufahasa.


Aliimba wimbo wa I Will Always Love you ambapo alijikuta akipewa zawadi kadhaa kutokana na umakini wake katika kuimba.


Jarida la Bang lilianzishwa mwaka 2004 ambapo limekuwa likijihusisha na kusaidia wasanii pamoja na masuala mengine katika jamii.


Mkurugenzi wa Jarida Hilo Emelda Mwamanga alisema kuwa kwa miaka 10 limesaidia mengi katika tasnia ya michezo, sanaa na mengineo.
================================

Related

Lilian Madeje aja na mradi wa kusaidia wakulima kufanya kilimo kiteknolojia akishirikiana na TBL

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Roberto Jarrin akizungumzia nafasi ya TBL katika kuwaendeleza wakulima nchini kiteknolojia ZaidiAdd caption Mwanzilishi mwenza wa mradi ...

TBL, Bits and Bytes wahamasisha wakulima kutumia Teknolojia na Ubunifu kuendelea kilimo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Roberto Jarrin akizungumzia nafasi ya TBL katika kuwaendeleza wakulima nchini kiteknolojia ZaidiAdd caption Mwanzilishi mwenza wa mradi ...

PiMAK yafungua duka Dar

Mmiliki wa kampuni hiyo, Riza Ergun akiwa na wadau kadhaa waliojitokeza kwenye uzinduzi huo Wafanyakazi na wageni waliojitokeza siku hiyo ya uzinduzi wa duka Riza Erguna akikata utepe k...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:

item