Makala: Ubunifu wa mavazi nchini






 Na Evance Ng’ingo
SEKTA ya mavazi ni moja kati ya sekta za kiutamaduni ambazo zinazidi kukua kwa kasi huku changamoto kubwa ikiwa ni kulipata vazi la taifa.

Sio suala geni kusikika masikioni mwa watu wakizungumzia upatikanaji wa vazi hilo la taifa kwa kwa kumekuwa na michakato mbalimbali iliyokwishawahi kufanywa na wadau mbalimbali katika kulipata vazi hilo.

Lakini pia katika kuendeleza utamaduni huo wa upatikanaji wa vazi hilo kumekuwa na maonesho mbalimbali ya mavazi ambayo yamekuwa yakifanyika sambamba na kuendeleza utamaduni wa mavazi chini.

Maonesho kama Lady in Red, Swahili Fashion, Usiku wa Kanga za Kale, Malaika na mengineo yotee yanalenga kukuza utamaduni huo wa mavazi.

Ili kuendeleza utamaduni huo kuna wabunifu mbalimbali ambao kila kukicha wamekuwa wakibuni mavazi kulingana na uhitaji wa soko kwa wakati husika.

Mbunifu Evelyn Rugemalila wa Eve Collection anasema kuwa kwa sasa soko kubwa lipo kwenye nguo za maharusi pamoja na sherehe za Kitchen Party mahsus kwa akina mama.
Anasema kuwa kwa upande wake anaona kuwa fursa katika soko hilo ndio inatoa mwanya wa ajira kwa watu wengi kwa sasa wanaojishughulisha na kazi za ubunifu.
Anasema kuwa wanadada wengi kwa sasa wanatambua kazi za wabunifu wa ndani na wamekuwa wakiwatumia katika kuwashone nguo zao za kibunifu.
Anaongeza kuwa kwa upande wake amekuwa akipata fursa za kuwashonea wanawake wengi hasa katika hafla mbalimbali.
“Inatakiwa kuwepo kabisa na sera kwanza ya kulinga hakimiliki ya kazi ya mbunifu wa mavazi hasa katika kutambua kazi zao, lakini pia inatakiwa kwa wabunifu pia kuzidisha ubunifu wa kazi ili kuendeleza tasnia hii inayokua kwa kasi hapa nchini”anasema Evelyn.

Ili kuendelea kuwa na wabunifu wakubwa wa mavazi hapa kama akina Mustapha Hasanali, Evelyn Rugemalila na wengineo inatakiwa pia kuwepo na mikakati endelevu ya kuwavumbua na kuwaendeleza wabunifu chipukizi hapa nchini.

Wapo wabunifu ambao mbali na kuwa na vipaji lakini havijaonekana na kufanyiwa kazi ipaswavyo na kuwawezeesha kuchangia kikamilifu maendeleo ya tasnia hiyo.

Mratibu Wiki ya Mavazi ya Swahili Fashion, Honest Arroyal anasema kuwa kupitia wameanzisha shindano la la kuvumbua vipaji lijulikanalo kama  Emerging Designer Awards.

Anaongeza kuwa ni katika shindano hilo ambapo wabunifu chipukizi wanaonesha uwezo wao katika ubunifu wa mavazi na kasha anachaguliwa mbunifu mmoja ambae ndio anatangazwa kuwa ni mshindi.

Anasema kuwa chini ya utaratibu kama huo wabunifu kama akina, Martin Kadinda, Pooja Jeshang, Sara Mosengo Aly Salim wa Mkoto Design na wengineo wamepatikana.

Anafafanua kuwa kwa mwaka huu ambapo onesho hilo litafanyika  Desemba 6, 7 na 8 pia kutakuwa na shindano kwa ajili ya wabunifu chipukizi.

Anaongeza kuwa hadi sasa wabunifu wengi wameshajitokeza na kuchukua fomu za ushiriki ikilinganiwa na miaka ya nyuma.

“Najua ili kukuza utamaduni huu wa mavazi na kuipa tasnia hii heshima inayostahili inatakiwa kuwepo kwa mikakati ya kisasa kabisa ya kuwaibua wabunifu na Swahili Fashion ndipo mahala pake”anasema Arroyal.

Kwa upande wake Martin Kadinda anasema kuwa kupitia maonesho ya mavazi ndipo vipaji vingi vinaibuliwa na kuwatengenezea mwanya wa ajira vijana.
Anaongeza kuwa anaona kuwa kwa sasa hata wasanii wamekuwa wakivalia nguo za wabunifu wa mavazi wa hapa hapa nyumbani.
Anaongeza kuwa kwa kufanya hivyo inaonesha ni kwa kiasi gani tasnia hiyo ya ubunifu wa mavazi inahusiana na sanaa ya muziki kwa ukaribu zaidi.

“Kwa mimi binasfi nilikua nikimvalisha msanii Nasib Abdul, Diamond kwa kipindi kirefum, na amekuwa akionekana nadhifu tena vema sana, hiyo ni kwa kazi yangu mimi kama mbunifu wa mavazi”anasema Kadinda.

Anaongeza kuwa kwa wasanii wa Marekani na kwengineko duniani hali imekuwa ni tofauti kwa kuwa wao wenyewe wanauza nguo zao na wanapata mabilioni ya fedha.
Hilo linajidhihirisha kwa msanii  mahiri wa Marekani ambae leo anatumbuiza  kwenye Tamasha la Serengeti Fiesta mwaka T.I.
Msanii huyo anamiliki mavazi yenye lebo mbalimbali kama vile Hustle Gang, Akoo pamoja na Strivers Row ambayo yameanza kuuzwa kwenye duka la Pop Up Shop lililopo Super Market ya Dar Free Market.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Grand Hustle Records, Jason Geter ambayo ndio kampuni inayomsimamia msanii B.O.B na mwanadada anayekuja kwa kasi Iggy Azalea wa Marekani, anasema anaamini soko la Tanzania na Afrika kwa ujumla ni masoko makubwa kwa bidhaa zao.
*                     
‘Tuna matarajio makubwa kuhusiana na kuleta bidhaa zetu nchini Tanzania, na tunatarajia sio tu kuleta bidhaa zetu hapa nchini, bali kwenda mbali zaidi kwa kujifunza soko la mitindo hapa nchini’ anasema Geter.
Anaongeza kuwa wasanii wanatakiwa kutumia umaarufu wao katika kujitafutia vyanzo vingine vya biashara muhimu.
=============

Related

Sticky 8573492956562391919

Post a Comment

emo-but-icon

item