Benki ya Twiga yaingia Kariakoo

Tawi la Twiga Bancorp Kariakoo



Na Mwandishi Wetu
WAFANYABIASHARA wa Kariakoo wametakiwa kutumia zaidi huduma za kibenki zipatikanazo katika eneo hilo ili kurahisisha uwekaji na utoaji wa fedha kwa ajili ya maendeleo ya biashara zao.
Mwito huo umetolewa na Afisa Mtendaji Mkuu wa benki ya Twiga, Cosmas Kimario wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na uamuzi wa benki hiyo kufungua tawi lake Kariakoo.
Alisema, Kariakoo ina mzunguko mkubwa wa fedha ambao wafanyabiashara wakubwa na wadogo wamekuwa wakisaidia mzunguko huo.
Alisema kuwa kutokana na hali hiyo benki zimekuwa zikiwekeza zaidi katika sekta hiyo na kuwa zimekuwa zikiendeleza wafanyabiashara hao katika uhifadhi wa fedha zao.
“Kwa sasa tunabiashara kubwa pale Kariakoo ambayo lazima tuweke tawi. Biashara yetu kubwa ni utoaji wa mikopo kwa uharaka kwa wafanyabiashara mbalalimbali, ubadilishaji fedha za kigeni, utumaji wa fedha nje ya nchi” alisema Kimario.
Aliongeza, Twiga ikiwa ni Benki ya serikali jukumu lake kubwa la kwanza ni kuhakikisha inchangia ukuaji wa uchumi kwa kuwezesha biashara kuendela zaidi, kuinua sekta isiyo rasmi kupitia mikopo ya vikundi, kuwapatia huduma bora za kibenki wananchi pale walipo ili kuongeza na kupanua wigo wa matumizi ya tasisi za kifedha kwa watanzania.
Aliongeza kuwa kwa ufunguzi huo wa tawi Kariakoo, Twiga Bancorp itakuwa imewafikia wananchi wengi wa eneo hilo hususani wafanyabiashara ambao wamekuwa wakitembea kufuata huduma zetu upande wa mjini kati Dar es Salaam na kuwanyima fursa baadhi ya wateja kutoka maeneno ya Kariakoo, Ilala, na viunga vyake.
"Ufunguzi wa tawi hili ni hatua mojawapo ya utekelezaji wa agizo la serikali lililoitaka benki hii kujitanua zaidi katika utoaji wa huduma zake, kuimarisha utendaji, na sisi tumeitikia kwa kuendelea na upanuzi wa huduma zetu kwa watanzania ambao kimsingi ni benki yao hii" alisema Kimario.
=============

Related

Technology 1175110146279873806

Post a Comment

emo-but-icon

item