BOA banki yajumuika na wagonjwa wa CCBRT

Wasanii wa kundi la Claudia wakicheza na wagonjwa waliolazwa kwenye hopsitali ya CCBRT wakati walipoenda hospitalini hapo kuburudisha, hafla hiyo iliandaliwa na Benki ya Afrika, Boa

Meneja wa Maendeleo ya Biashara wa Benki of Afrika, BOA, Wasia Mushi akikabidhi vifaa vya masomo kwa watoto waliolazwa kwenye hospitali ya CCBRT ikiwa ni sehemu ya kusherehekea sikukuu ya Pasaka na watoto hao



Meneja wa Maendeleo ya Biashara wa Benki of Afrika, BOA, Wasia Mushi akiwahudumia chakula watoto waliolazwa kwenye hospitali ya CCBRT ikiwa ni sehemu ya kusherehekea sikukuu ya Pasaka na watoto hao


Meneja wa Maendeleo ya Biashara wa Benki of Afrika, BOA, Wasia Mushi akikabidhi misaada ya aina mbalimbali kwa watoto waliolazwa kwenye hospitali ya CCBRT ikiwa ni sehemu ya kusherehekea sikukuu ya Pasaka na watoto hao

habari kamili.

Na Mwandishi Wetu, Evance
JAMII imetakiwa kuendelea na moyo wa kuwasaidia wagonjwa wa aina mbalimbali hasa watoto hususan kwenye kipindi cha sikukuu kama vile Pasaka na nyinginezo.
Wito huo ulitolewa juzi na Meneja wa Maendeleo ya Biashara wa Benki of Afrika, BOA, Wasia Mushi wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Hospitali ya CCBRT ambapo wafanyakazi wa benki hiyo walioenda kusherehekea sikukuu ya Pasaka na wagonjwa.
Alisema kuwa wagonjwa wanahitajia faraja kutoka kwa watu mbalimbali na wao wakiwa kama wafanyakazi wa benki wameona kuwa ni vema wakatumia sikukukuu hiyo kusherehekea na wagonjwa hao.
"Hii ni sikukuu kubwa tena sana lakini wakati watu tukiwa majumbani mwetu na watoto wetu tutambue kuwa wapo watoto na watu wengine wamelazwa na hawana nafasi ya kushiriki sherehe kama hizi" alisema Mushi.
Mushi alisema kuwa pia imekuwa ni wasaha mzuri kwa wafanyakazi wa benki hiyo kuungana na wazazi wa watoto hao ambao wanawauguza hospitalini hapo.
Wakiwa hospitalini hapo wafanyakazi hao wa benki waligawa zawadi mbalimbali kwa wagonjwa pamoja na kula nao chakula cha mchana.
Pia walitoa zawadi za vifaa vya kusomea kama madaftari, kalamu pamoja na mifuko ya kubebea vifaa hivyo.
Watoto pamoja na wazazi wao walipata nafasi ya kucheza michezo mbalimbali wakishirikiana na wafanyakazi wa benki hiyo.
Mama mzazi wa mtoto Joseph Mali, Maria, alisema kuwa kwa upande wake na mtoto wake wamefurahishwa na misaada hiyo na imekuwa ni faraja kubwa kwao.
"Tumecheza muziki tumefurahia na kujiona kuwa tupo pamoja na wenzetu yani hata mwanangu amefurahi na kujikuta akila na kushiba kabisa". alisema Maria.

=========


Related

Technology 6533216206701937107

Post a Comment

emo-but-icon

item